Home » » MTUHUMIWA WA UBAKAJI ATIWA MBARONI

MTUHUMIWA WA UBAKAJI ATIWA MBARONI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

JESHI la Polisi mkoani Pwani limefanikiwa kumkamata Michael William maarufu (Michael dada), mkazi wa Kiluvya, wilayani Kisarawe anayetuhumiwa kuhusika na matukio ya ubakaji wa vikongwe mkoani hapa.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Ulrich Matei alisema jeshi hilo lilikuwa likimsaka mtuhumiwa huyo kwa kipindi kirefu kutokana na kudaiwa kutenda makosa mbalimbali ya ubakaji wa vikongwe na wanawake na kutokomea kusikojulikana.
Alisema, William alitiwa mbaroni juzi baada ya kudaiwa kuhusika katika tukio la wizi wa mifugo lililotokea wiki mbili zilizopita huko Kiluvya.
Pia kamanda Matei alisema, mtuhumiwa huyo anadaiwa kuhusika katika matukio ya ubakaji zaidi ya 10 ambapo kabla ya kufanya vitendo hivyo alikuwa akiwatishia wahusika kwa mapanga.
“Huyu kijana anayejiita Michael dada ni maarufu kwa matukio ya ubakaji na alilisumbua jeshi letu mara kadhaa kwa kunasua mitego aliyowekewa leo tumelazimika kumleta mbele yenu waandishi ili mumuone ni mdogo lakini ametusumbua sana,” alisema.
William alikiri mbele ya waandishi wa habari kuwa miaka ya hivi karibuni aliwahi kufanya unyang’anyi wa kutumia silaha kosa ambalo lilimsababishia kuhukumiwa miaka 30 jela.
Matei alisema kabla kifungo hicho hakijamalizika mwaka 2011 na 2012, William alikata rufaa na kutolewa ili kuendelea na taratibu nyingine na tangu hapo hakuonekana hadi polisi walipofanikiwa kumkamata kwa kosa la wizi wa mifugo.
Hata hivyo William alikana kuhusika na tuhuma zinazomkabili na kudai yeye sio Michael dada kama anavyoitwa bali ni Michael William na tuhuma za ubakaji ni za kusingiziwa.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa