Home » » WAFANYABIASHARA WAMKATAA OFISA MISITU

WAFANYABIASHARA WAMKATAA OFISA MISITU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WAFANYABIASHARA wa mazao ya misitu wilayani Kisarawe, Pwani wameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Wakala wa Misitu Nchini (TFS) kumwondoa ofisa wake, Mathew Mwanuo na kuwaletea mwingine.
Mwanuo anatuhumiwa na wafanyabiashara hao kuwalazimisha watoe rushwa kila wanapokwenda msituni kuvuna mkaa na mazao mengine yatokanayo na misitu.
Akisoma maazimio ya pamoja baada ya kumaliza mkutano wao juzi, Katibu wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Mazao ya Misitu (Uwamami), Ally Kombo, alisema wanaitaka TFS imwondoe ofisa huyo.
Kombo alitaja sababu kubwa ya kutaka aondolewe ni kukosa imani na utendaji wa Mwanuo wa kulazimisha rushwa kwa kutafuta makosa ya uongo, ili apate chochote.
“Wafanyabiashara wenzangu baada ya kuwasikiliza kwa kina, niliwahoji kama mnataka tuendelee na hadha hii… wengi mlisema mnataka Mwanuo aondoke Kisarawe, hivyo tunaiomba TFS imwondoe ofisa huyo,” alisema.
Wafanyabiashara hao pia wamewataka maofisa wa Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) na Askari wa Jeshi la Polisi wanaopangiwa katika vizuizi viwili Pugu Kajungeni na Mwisho wa Lami kufuata sheria ya kazi na siyo kulazimisha makosa ili waandike faini.
Akizunguma na Tanzania Daima kuhusu tuhuma hizo, Mwanuo alisema si kweli na kwamba atayashughulikia malalamiko hayo kwa kukaa na viongozi wa wafanyabiashara hao pindi atakaporejea kutoka likizo.
“Yaliyoelezwa na wafanyabiashara hao si ya kweli, ni uzushi mtupu… nipo likizo na ninatarajia kurejea ofisini Julai 17 mwaka huu, nikirudi tu nitawaomba viongozi tuzungumze,” alisema Mwanuo.
Meneja wa Kanda ya Mashariki wa TFS, Bakari Mohamed, alisema ofisi yake haijapelekewa malalamiko yoyote na kwamba atatafuta nafasi ya kukaa na wafanyabiashara wote waeleze tatizo lilipo, ili walimalize
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa