Home » » WAKAZI KIBAHA WAAZIMIA KUGAWANA SHAMBA

WAKAZI KIBAHA WAAZIMIA KUGAWANA SHAMBA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
ZAIDI ya wakazi 300 wa mitaa ya Viziwaziwa, Mikongeni na Sagale, wilayani Kibaha, wameazimia kugawana shamba la 117, mali ya Saeni ambaye amelitelekeza kwa zaidi ya miaka 22 sasa.
Shamba hilo ambalo lipo katika mitaa hiyo limekuwa chanzo cha wanafunzi wengi kukatisha masomo  kutokana na kufanyiwa vitendo vya ubakaji na hatimaye kupata mimba, huku vitendo vya mauaji na uporaji vikifanyika katika eneo hilo ambalo limekuwa na pori kubwa.
Wakizungumza kwenye mkutano wa pamoja wakazi wa vijiji hivyo chini ya uongozi wa muda wa Mwenyekiti Shabani Matimbwa, walisema wamekuwa wakijadili changamoto hiyo kwenye mikutano halali ya mitaa yao, lakini viongozi waliopo madarakani hawachukulii uzito suala hilo wala kulitolea majibu kwenye mikutano.
Akizungumza kwenye mkutano huo ambao uliwashirikisha wananchi wa mitaa hiyo waliounda umoja wao wa  mitaa hiyo ‘Vimisa’, mwenyekiti  huyo wa muda alisema walikubaliana kuwaita Diwani wa Kongowe, Salum Bagumeshi, mwenyekiti wa mitaa hiyo, mtendaji na kiongozi wa polisi kata, ili kufikia muafaka wa kuligawa shamba hili na kujenga shule ya sekondari, upanuzi wa zahanati, soko pamoja na kutenga eneo la kiwanja cha michezo.
Wananchi  hao walikubaliana kutenga ekari 30 kwa ajili ya mambo ya maendeleo, na ekari zilizobakia kugawana kila mmoja aliye ndani ya ‘Vimisa’ aweze kupata eneo la kulima na wengine kujenga kwa maendeleo yao.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa