Home » » UVCCM YAANDAA MKAKATI KUJIIMARISHA

UVCCM YAANDAA MKAKATI KUJIIMARISHA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

JUMUIYA  ya Vijana wa Chama Cha Mapinduzi  (UVCCM) Wilaya ya Kibaha Mjini, kwa kushirikiana na makatibu 11 wa kata zote wilayani hapa, wameandaa mpango mkakati wa kuimarisha uhai wa jumuiya hiyo, ili iweze kutekeleza majukumu yake ya kila siku.
Katibu wa UVCCM wilayani hapa, Khalid King, alisema lengo ni kuongeza wanachama wapya kwa kila kata na kuvuna wanachama 1,000 hadi itakapofika mwishoni mwa mwezi huu.
Alisema katika mkakati huo hadi sasa wameshapata wanachama wapya 400 kwa kipindi cha miezi mitatu na wanatarajia kupata zaidi ya wanachama 1,000 ndani ya mwezi huu.
King alitaja mpango mwingine ni kuunganisha vijana bila kujali itikadi za kisiasa ikiwemo wajasiriamali, madereva wa piki[iki ‘bodaboda’ kwa kutumia michezo na kuwaweka katika makundi, ili waweze kukopesheka. 
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa