Home » » TIMU YA MAISHA PLUS/MAMA SHUJAA WA CHAKULA YAICHABANGA GOLI MBILI KWA MOJA TIMU YA WAANDAAJI WA MAISHA PLUS/MAMA SHUJAA WA CHAKULA

TIMU YA MAISHA PLUS/MAMA SHUJAA WA CHAKULA YAICHABANGA GOLI MBILI KWA MOJA TIMU YA WAANDAAJI WA MAISHA PLUS/MAMA SHUJAA WA CHAKULA

 Timu ya kikosi cha waandaaji wa Kipindi cha Maisha Plus/ Mama  Shujaa wa Chakula wakiwa katika Picha ya Pamoja kabla ya Mechi kuanza dhidi ya Vijana wa Maisha Plus/ Mama Shujaa wa chakula
 Babu wa Kijiji cha Maisha Plus ambaye ndiye alikuwa Refalii wa Mchezo huo
 Baadhi ya Mashabiki wa Timu ya Waandaaji wa Kipindi cha Maisha Plus/ Mama Shujaa wa Chakula wakiwa wanashauriana na Kufuatilia mtenange kwa umakini zaidi.
 Mtenange ukiwa unaendelea
 Mashabiki wa timu ya Maisha Plus/ Mama Shujaa wa Chakula wakiwa wanashangilia Ushindi wao baada ya kuwachabanga Magoli mawili kwa moja timu ya Waandaaji wa kipindi hicho cha Maisha Plus Mama Shujaa wa Chakula mechi iliyochezwa katika Kijiji cha Maisha Plus.
******

Kulikuwa na mambo mengi sana katika Kijiji cha Maisha Plus ambapo walipata Ugeni Mkubwa wakawa na michezo mingi lakini Furaha iliendelea kufana zaidi pale timu ya mpira wa miguu ya kijiji cha Maisha Plus ilipopata ushindi wa mabao 2–1 dhidi ya wafayakazi na waandaaji wa kipindi cha Maisha Plus na Mama Shujaa wa Chakula 2014. Magoli yote yalifungwa katika kipindi cha kwanza huku timu ya wafanyakazi ikiongoza kwa goli moja huku timu ya kijiji cha Maisha Plus kusawazisha na baadaye kuongoza kwa goli moja na kuwa washindi. Kwa upande wa wafanyakazi goli lilifungwa na Erick Mlindima huku timu ya kijiji goli la kusawazisha lilifungwa na Boniphace Meng’anyi mwenye namba ya ushiriki MP 06 huku goli la ushindi lilifungwa na Said Rashid mwenye namba ya ushiriki MP 29.
 


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa