Siku hii ni yenye balaa kwa
wanakijiji cha Maisha Plus kutokana na matukio yaliyotokea ambayo matokeo yake
si mazuri kwa wanakijiji hao. Awali ya yote asubuhi kama kawaida walifanya
usafi wa mazingira na kaya zao huku wanakijiji wengine wakiongea na babu
kuhusiana na kilichojiri kijijini hapo. Kulikuwa na uvumi ya kwamba kuna
mwanakijiji mmoja asiyetambulika anawachawia wenzake usiku wanapolala
pasipokujua ni nani anayefanya hivyo.
Baadhi ya wanakijiji hao walikuwa
wakimshuku kijana Boniphace Meng’anyi kuwa inawezekana ikawa ni yeye ingawa
hawakuwa na ushahidi wowote bali wanahisi tu. Hii inatokana na kwamba kijana
huyo hana uwoga na huwa na desturi ya kwenda kisimani usiku kuoga na kufanya
shughuli zake nyingine.
Tabia ya kijana huyu iliwafanya baadhi ya wanakijiji
kuwa na wasiwasi naye zaidi kuhusika na kitendo hicho ingawa mpaka sasa hawana
uhakika wa mtu anayehusika kuchawia wenzake usiku walalapo.
Pamoja na matukio mengine
kutokea hapo kijijini haikuwazuia wanakijiji kubadilishana mawazo na kujadili
masuala mbalimbali yanayowahusu. Mambo mbalimbali yalijadiliwa ikiwa ni pamoja
na malengo waliyokuwa nayo wanakijijii baada ya kutoka hapa katika kijiji cha
Maisha Plus.
Wengi wao waliahidi kuendeleza walichokipata kwa kuelimisha jamii
inayowazuka, kujiajiri kwa vijana na kupanua miradi waliyokuwa nayo ili waweze
kupiga hatua katika kujiletea maendeleo.
Mama Shujaa wa Chakula walichukua
fursa hii kuwasisitiza watoto wao kujishughulisha na kilimo kwani kinaleta tija
kwa mkulima na taifa kwa ujumla badala ya kuzurura mitaani na kukaa vijiweni.
Kizaa zaa kilitokea kijijini
baada ya yai walilokabidhiwa wiki kadhaa zilizopita kuvunjika. Yai hilo lina
historia ndefu ambapo hapo awali yai lilifichwa na atakaye bahatika kulifichua
litamlinda kwa maana hatatoka kwenye mashindano hata kama atakuwa kwenye orodha
ya mchujo.
Farida Ally kutoka Pwani alifanikiwa kupata yai la kwanza lakini kwa
bahati mbaya lilivunjika baada ya kukaa nalo kwa siku chache hivyo kuingia moja
kwa moja katika orodha ya mchujo.
Kwa kuwa walitakiwa washiriki watano kuaga
mashindano hayo kipindi hicho naye alikuwa miongoni mwa waliotolewa iliyofanya
washiriki wengine kuwa makini katika kufanya maamuzi wa jambo kama hili.
Baada
ya yai hilo kuvunjika siku ya pili yake lililetwa yai jingine ambapo nafasi
ilitangazwa kwa aliyetayari kulitunza na lenyewe kumlinda asiweze kutoka katika
kinyang’anyiro cha Maisha Plus 2014.
Wanakijiji walifanya jitihada zote kulinda yai hilo lisije kuvunjika na wakati mwingine wanakijiji hao hawalali usiku kuhakikisha lipo salama.
Jitihada za wanakijiji ziligonga mwamba pale yai lilipovunjika kutokana na joto lililopo kwani lilikuwa katika sehemu ya uwazi ambapo hukabiliwa na mvua, jua na baridi.
Yai hili lilisadikika kuvunjika siku mbili au tatu zilizopita ila wanakijiji walipata hofu kubwa baada ya kusikia taarifa hizo kwani walijua kabisa tayari wapo matatani na wameshazua balaa kijijini hapo hivyo kusita kutoa taarifa kwa wahusika na kukaa kimya.
Balaa watakalopata ni kukaa na njaa na kupewa adhabu ambayo hawaijui itakuwa ni ya aina gani hivyo kuzidisha hofu zaidi miongoni mwa wanakijiji. Babu na Masoud Kipanya wameshasikia habari za kuvunjika kwa yai kijijini na haieleweki ni hatua gani watakayoichukua
0 comments:
Post a Comment