Home » » KINA MAMA KIBAHA WATAKIWA KUACHAUTEGEMEZI

KINA MAMA KIBAHA WATAKIWA KUACHAUTEGEMEZI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
KINA mama nchini wametakiwa kuachana na tabia ya kuwa tegemezi na badala yake  wajiunge katika  vikundi vya ujasiriamali  kwa lengo la kupamabana na umasikini.
Rai hiyo ilitolewa mjini hapa jana na mjumbe wa Kamati ya Uekelezaji ya Umoja wa Wanawake Wilaya ya Kibaha kupitia CCM, Elina Mgonja wakati wa ziara ya UWT ya kuwatembelea kina mama hao kwa lengo la kubaini changamoto zinazowakabili.
Mgonja alisema kwamba kwa sasa kina mama wanatakiwa kuwa na mtazamo chanya wa kuelekeza nguvu zao kushiriki kufanya kazi, hali ambayo itaweza kuwaletea mabadiliko makubwa.
“Wanawake inabidi kuwa na mshikamano wa hali ya juu katika kushirikiana katika majukumu mbalimbali, na kikubwa kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali ambavyo nina imani vitakuwa mkombozi kwenu,” alisema.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wilaya ya Kibaha, Mwanaidi Kiongoli, aliwataka kina mama hao kutokuwa waoga katika kufanya uamuzi, kwani kufanya hivyo wanajirudisha nyuma.
Chanzo;anzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa