Home » » DIHOZILE WALIA KERO YA MAJI

DIHOZILE WALIA KERO YA MAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mgombea ubunge Chalinzr kwa tiketi ya CCM, Ridhiwani KikweteWAKAZI wa Kijiji cha Dihozile, Kata ya Msoga, wilayani Bagamoyo, wanatembea umbali wa zaidi ya saa mbili kupata huduma ya maji.
Wakizungumza katika mkutano wa kampeni wa mgombea ubunge  kwa tiketi ya CCM, Ridhiwani Kikwete, wakazi hao walisema adha hiyo imekuwa ikisababisha wakati mwingine kushindwa kufanya shughuli za maendeleo.
Akizungumza na wananchi wa kijiji hicho, Ridhiwani, aliwaomba wananchi hao kumchagua ili ashughulikie kero hiyo.
Ridhiwani aliahidi endapo atachaguliwa kuwa mbunge atajenga visima viwili vya pampu ili kutatua changamoto hiyo.
Katika hatua nyingine, Ridhiwani aliahidi kumsomesha kijana Abdala Salehe, mkazi wa Kijiji cha Tonga kuendelea na masomo  endapo watamchangua kuwa mbunge.
Abdala alifaulu katika Shule ya Sekondari Bagamoyo, lakini ameshindwa kuendelea na masomo kutokana na kukosa watu wa kumsaidia.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa