USHURU wa mabango na kodi nyingine zinazotozwa kwa wafanyabiashara
wa mji wa Mailimoja zimeelezwa kuwa ni changamoto kubwa kwa
wafanyabiashara.
Akizungumza wakati akikabidhi zawadi mbalimbali kwa wateja walionunua
simu kwenye duka la Kampuni ya Lipwai lililopo Mailimoja mjini hapa,
Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Mohamed Lutambi, alisema kodi hizo ndizo
hasa zinazowakwamisha baadhi yao kuendelea kibiashara.
Lutambi alisema kodi kubwa za leseni za biashara, ushuru wa biashara
pamoja na ushuru wa mabango bado ni changamoto kubwa kwao kutokana na
kutumia fedha nyingi kulipa kodi kwenye biashara wanazoendesha.
Alisema malengo ya kampuni hiyo ni kufanya biashara kubwa katika mji
huo kwa kuwawezesha wakazi wa Mailimoja kupata mahitaji yote wanayofuata
nje ya mji huo.
Alieleza wakati wakianzisha biashara hiyo mwaka 2004 walikumbana na
changamoto ya soko pamoja na upatikanaji wa mitaji ambapo Benki ya NMB
iliwasaidia kukabiliana na changamoto hiyo kwa kuwapa mikopo ambayo
iliwasaidia kuinuka kiuchumi.
Ofisa Maendeleo ya Jamii wa mji wa Kibaha, Novman Gimbi, aliwasihi
vijana kuchangamkia fursa zilizopo kwa kufika katika ofisi za
halmashauri, ili waweze kunufaika na mikopo inayotolewa endapo kijana
atakuwa amejiunga na Chama cha Akiba na Mikopo (Saccos).
Katika hafla hiyo zaidi ya wateja 20 walizawadiwa zawadi mbalimbali zikiwemo simu za mikononi, vocha na zawadi nyingine
Chanzo;Tanzania daima
0 comments:
Post a Comment