Ni kwa asilimia 90 wilayani Bagamoyo, baada ya kuanzisha mpango wa kugawa fedha kwa a maskini.
Bagamoyo.
Zaidi ya asilimia 90 ya wanafunzi wanaopata mimba katika Shule za Msingi na Sekondari wilayani hapa Mkoa wa Pwani, imepungua kufuatia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) kutoa pesa kwa kaya maskini.
Zaidi ya asilimia 90 ya wanafunzi wanaopata mimba katika Shule za Msingi na Sekondari wilayani hapa Mkoa wa Pwani, imepungua kufuatia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) kutoa pesa kwa kaya maskini.
Mfuko huo wa maendeleo ambao upo katika awamu ya
tatu ya utekelezaji wake, imekuwa ikisaidia kaya maskini katika mpango
wao wa uhawilishaji fedha ambapo kaya hizo hugaiwa fedha kila mwezi kwa
ajili ya kupunguza umaskini.
Tatizo la mimba na utoro wilayani humo pamoja na
mambo mengine limeelezwa kuchangiwa na wazazi wengi kutokuwa na kipato
cha uhakika hivyo kushindwa kuwapatia watoto wao mahitaji muhimu na
kujikuta wakitumbukia katika vitendo viovu ikiwamo matumizi ya dawa za
kulevya na mimba.
Mwenyekiti wa Kijiji Fukayosi, Salum Mkecha
alibainisha hayo wakati Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi
alipotembelea miradi inayofadhiliwa na Tasaf wilayani humo.
Kwa mujibu wa Mkecha, tatizo la mimba limepungua
tangu mradi huo umeanza na kwamba mpaka sasa hajapokea taarifa hata moja
ya ujauzito kutokana na wananchi kupata mahitaji ya msingi jambo
alilodai linachangia hata wananchi hao kupata huduma za afya pindi
wanapougua.
Alisema wanafuzi wengi walikuwa wakipata mimba kwa
kukosa mahitaji ya msingi na kujikuta wakishindwa kuendelea na masomo
huku wavulana wakijitumbukiza katika vitendo viovu kama matumizi ya dawa
za kulevya lakini sasa hali ni tofauti.
Mkuu wa Wilaya hiyo Ahmed Kipozi aliwataka
wananchi hao kuzitumia kwa manufaa yao fedha hizo ikiwamo kujiunga na
huduma za msingi kama bima ya afya. maendeleo,”alisisitiza Kipozi.
ChanzoMwananchi
ChanzoMwananchi
0 comments:
Post a Comment