Home » » WAKULIMA WALIA NA MIFUGO

WAKULIMA WALIA NA MIFUGO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

WAKULIMA kwenye mashamba yaliyopo katika vitongoji vilivyomo ndani ya Kijiji cha Kidogozero, Kata ya Vigwaza Bagamoyo Mkoa wa Pwani wamauomba uongozi mkoani humo kusaidia ili kuondokana na kero ya mifugo inayoingia kwenye mashamba.

Wakazi Bw.Said Msumi na Ally Mwenda kwa niaba ya wenzao waliwaeleza waandishi wa habari kuwa kero hiyo imekuwa kubwa kiasi cha kuwakatisha tamaa kwenye kuendeleza kilimo.

"Kama mnavyoyaona makundi yamifugo hii ndio hali halisi kila kukicha hali iko hivi,hatuna raha yakuendelea nakilimo kutokana na mifugo kwani imekuwa kero kubwa,tunawaomba viongozi ngazi ya mkoa watusaidie," alisema Msumi.

Aliongeza kwamba,kutokana na ukweli huo unapofika wakati wa kilimo wanalazimika kutumia zaidi ya sh. lakimoja kwa ajili ya kuingiza trekta badala ya sh.50,000 kwa eka hii hiyo inatokana na ardhi kuwa ngumu hatua ambayo wamiliki wa vyombo hivyo kutoza kiasi hicho.

Kwa upande wake Mwenda alisema wachungaji wanaingiza mifugo katika mashamba hali inayotishia usalama kwenye maeneo hayo na jamii hiyo inayojihusisha na mifugo.

" Hii hali inatisha sana hivyo tunawaomba viongozi ngazi ya mkoa wa wafike kutusaidia ili nasi tuwe na uhuru wakutekeleza kilimo chetu ambacho ndio tunachokitegemea katika kuendesha maisha yetu," alisema Bw. Mwenda .

Akizungumzia changamoto hiyo mwenyeki ti wa kijiji hicho Bw.Ally Mmanga amekiri kuwepo kwa hali hiyo nakueleza wamewasiliana na uongozi wa NAFCO uli opojirani kabisa na kijiji ili kusaidia na kudhibiti hali hiyo

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa