Home » » VIONGOZI WATAKIWA KUTOPUUZA TAASISI ZA DINI

VIONGOZI WATAKIWA KUTOPUUZA TAASISI ZA DINI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

VIONGOZI wa Serikali, wametakiwa kutopuuza mialiko kutoka Taasisi za kidini kwani katika shughuli hizo za kijamii hutumika kufikisha changamoto zao ambazo zinahitaji ufumbuzi.
Ombi hilo limetolewa mjini Kibaha juzi, wakati wa sherehe za Baraza la Idd zilizofanyika katika Taasisi ya kidini inayojishughulisha na kutoa huduma ya elimu na kusaidia makundi mbalimbali ya WIPHAS, na Mwenyekiti wa maandalizi ya baraza hilo, Mohamed Kiaratu.
Kiaratu, aliwaambia waandishi wa habari kuwa, viongozi wa serikali ni muhimu kushirikiana na wananchi hasa pale wanapopewa mialiko, kwani wao wana ufafanuzi wa mambo mbalimbali ambayo ni changamoto kwenye Taasisi.
“Viongozi wa serikali wanatakiwa wasitupuuze, wanapopata mialiko yetu wajitahidi kushiriki pamoja na sisi, kwani tuna mambo mengi ya kuwakilisha kwao ambayo tunaamini wao ndio wenye ufafanuzi wa kina,” alisema Kiaratu.
Akizungumzia suala la ujenzi wa ofisi ya Bakwata Mkoa wa Pwani, aliwaomba wadau mbalimbali kuchangia ili kufanikisha lengo hilo, ambako hadi sasa ujenzi huo umegharimu sh milioni 200 huku ikihitajika milioni 300 kukamilisha.
Akihutumia mamia ya wakazi wa Kibaha waliohudhuria baraza hilo, Mbunge wa Mafia, Abdukarim Shaha, alitoa wito kwa Taasisi hiyo kutafuta namna ya kufungua vituo vingine ili huduma wanayoitoa ifikie katika mikoa mingine ya jirani.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa