MHE. RIDHIWANI KIKWETE AONGOZA MAMIA YA WANANCHI WALIOJIAJIRI KUJIUNGA NA KUJIWEKEA AKIBA NSSF
WANANCHI WALIOJIAJIRI CHALINZE WACHANGAMKIA KUWA MASTAA WA MCHEZO WA NSSF
DC MAFIA AZINDUA UVUNAJI WA JONGOO
Uvunaji huo wa jongoo bahari umezinduliwa rasmi kwa mara ya kwanza ambapo Mhe. Mangosongo amempongeza mfugaji wa jongoo bahari, mzee Mpogo kwa mchango wake wa kendeleza uchumi wa buluu pamoja na kuleta fursa ya ajira kwa vijana.
" Tumevutiwa sana, vijana wengi wangepatiwa elimu na kujishughulisha na ufugaji wa jongoo bahari, basi wangejikwamua na tatizo la ajira. Kwa upande mwengine, mradi huu unatunza mazingira na ndivyo ambavyo viongozi wetu, hasa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anavyotutaka kujikita katika uchumi wa buluu na kutunza mazingira" alisema Mhe. Mangosongo.
Kwa upande wake, Mfugaji wa jongoo bahari Mzee Waziri Mpogo, ameipongeza Serikali kupitia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Halmashauri kwa kutoa ushirikiano kuwezesha fursa hiyo kuwepo pamoja na kuwaomba wakazi wa Mafia wajitokeze kufanya shughuli hiyo ili kuifungua wilaya zaidi kwenye suala la uchumi wa buluu.
Lengo langu ni kutaka wafugaji wadogo wadogo waweze kupata mbegu hapahapa Wilayani badala ya kuzifuata Bagamoyo ama sehemu nyingine" alisema Mzee Mpogo. Nimepata faraja pia kuona mazingira yapo salama kwa sababu mradi huu unasaidia kutunza mazingira, hivyo nawaomba viongozi na wananchi wote tushirikiane katika kukuza uchumi wa buluu" aliongeza.
Mradi huo uliogharimu Shilingi Milioni 176, umekuwa msaada kwa vijana kwa kuwasaidia kuwapa fursa ya ajira.
" Nawaomba vijana wenzangu kujitokeza katika mradi huu badala ya kujishughulisha na mambo ya uhalifu, tunaweza pia kuunda kikundi chetu na kujikwamua kiuchumi" alisema Salum Alawi, kijana anayefanya kazi katika kampuni ya Mpogo Ocean Ranching inayojihusisha na ufugaji wa jongoo bahari.
Mbunge wa Chalinze ameshiriki kikao cha Baraza la Madiwani Cha Chama Cha Mapinduzi kuchagua Diwani
MA DC WAJENGEWA UWEZO KUSIMAMIA UTOAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10
Na. James Mwanamyoto, OR-TAMISEMI
Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - TAMISEMI Bw. Sospeter Mtwale amesema Wakuu wa Wilaya wanapatiwa mafunzo na Ofisi ya Rais -TAMISEMI ya kuwajengea uwezo wa kusimamia zoezi la utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri za Wilaya kwa akina mama, vijana na wenye ulemavu.
Bw. Mtwale amesema hayo leo katika Ukumbi wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha mkoani Pwani kwa Niaba ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - TAMISEMI Bw. Adolf Ndunguru wakati akifungua kikao kazi cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa na Wakuu wa Wilaya zote nchini.
Bw. Mtwale amesema, Serikali imeanza kutoa mikopo ya asilimia 10 baada ya hapo awali kusitishwa kutokana na changamoto jilizojitokeza, na kuongeza kuwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI imeshapitia kanuni na kufanya maboresho na ikaona ni vema Wakuu wa Wilaya wakapitishwa katika kanuni hizo ili waweze kushiriki kikamilifu katika usimamizi wa utoaji wa mikopo hiyo.
“Tumeona ni vema nanyi mkapitishwa katika kanuni hizo ili tuwe na uelewa wa pamoja katika kusimamia utoaji wa mikopo hiyo ili mikopo hiyo iwe na tija kwa watakaonufaika na katika taifa kwa ujumla,” Bw. Mtwale amesisitiza.
Sanjali na hilo, Bw. Mtwale amesema Wakuu wa Wilaya watapitishwa katika taarifa ya ukaguzi ya mwaka wa fedha 2022/23 ili wafahamu hoja zilizoibuliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwani nao ni wasimamizi wa halmashauri zilizopo katika maeneo yao ya utawala.
Ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya Wakuu wa Wilaya nchini, Bw. Mtwale amesema Ofisi ya Rais - TAMISEMI imemualika mtaalamu wa afya ya akili kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dkt. Garvin Kweka ili kuwapatia elimu ya afya ya akili na ya namna bora ya kuepukana na magonjwa ya afya ya akili.
Akiwasilisha mada kuhusiana na afya ya akili, mtaalamu wa afya ya akili kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dkt. Garvin Kweka amewataka Wakuu wa Wilaya kuzingatia mahusiano ya kijamii ili kujenga afya nzuri ya akili itakayowawezesha kutekeleza kikamilifu majukumu yao kwa ufanisi.
“Mtu anayeenda kwenye jumuiya, vikoba, kanisani au msikitini akipata msiba, msiba wake hauwi sawa na mtu anayejifungia ndani hivyo mahusiano ya kijamii ni lazima yazingatiwe na kisingi ndio utulivu wa afya ya akili,” Dkt. Kweka amesisitiza.