MHE. RIDHIWANI KIKWETE AONGOZA MAMIA YA WANANCHI WALIOJIAJIRI KUJIUNGA NA KUJIWEKEA AKIBA NSSF

*Ni katika muendelezo wa kampeni ya elimu kwa umma kuhusu Skimu ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi Waliojiajiri Chalinze mkoani Pwani *NSSF yaahidi kufikisha elimu ya hifadhi skimu kwa wananchi wengi zaidiNa MWANDISHI WETU, PWANIWaziri wa Nchi,  Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Ridhiwani Kikwete amewaongoza mamia ya wananchi wa Chalinze mkoani Pwani, katika muendelezo wa elimu kwa umma kuhusu Skimu ya Taifa ya Hifadhi ya Jamii kwa Wananchi Waliojiajiri yenye jina la kampeni  "NSSF STAA WA MCHEZO".Akizungumza na wananchi waliojiajiri, mwishoni mwa wiki iliyofanyika Chalinze mkoani Pwani, Mhe....

WANANCHI WALIOJIAJIRI CHALINZE WACHANGAMKIA KUWA MASTAA WA MCHEZO WA NSSF

Tayari timu ya NSSF ipo mtaani katika Soko la Bwilingu na maeneo mengine ya Halmashauri ya Chalinze mkoani Pwani kwa ajili ya kutoa elimu ya hifadhi ya jamii, kwa wananchi waliojiajiri ambapo mwamko wa wananchi kujiunga na kujiwekea akiba umekua mkubwa.Tunaposema ‘Staa wa Mchezo’ ni wananchi ambao wamejiajiri kupitia sekta ya kilimo, ufugaji, uvuvi, madini (wachimbaji wadogo wadogo), usafirishaji (boda boda na bajaji), sekta ya biashara ndogo ndogo (Machinga, Mama/Baba lishe, ususi, muuza mkaa, muuza nyanya na staa wengine wote). Ujio wa ‘Hifadhi Scheme’ unatoa nafasi kwa NSSF kushika usukani na kuwa staa wa mchezo katika maisha ya uzeeni au...

DC MAFIA AZINDUA UVUNAJI WA JONGOO

Mkuu wa Wilaya ya Mafia, Mhe. Aziza Mangosongo amezindua uvunaji wa jongoo bahari katika kitalu kilichopo kijiji cha Dongo, kitongoji cha Mfuruni Julai 30, 2024.Uvunaji huo wa jongoo bahari umezinduliwa rasmi kwa mara ya kwanza ambapo Mhe. Mangosongo amempongeza mfugaji wa jongoo bahari, mzee Mpogo kwa mchango wake wa kendeleza uchumi wa buluu pamoja na kuleta fursa ya ajira kwa vijana." Tumevutiwa sana, vijana wengi wangepatiwa elimu na kujishughulisha na ufugaji wa jongoo bahari, basi wangejikwamua na tatizo la ajira. Kwa upande mwengine, mradi huu unatunza mazingira na ndivyo ambavyo viongozi wetu, hasa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anavyotutaka...

Mbunge wa Chalinze ameshiriki kikao cha Baraza la Madiwani Cha Chama Cha Mapinduzi kuchagua Diwani

 Mbunge wa Chalinze,Ridhiwani Kikwete ameshiriki kikao cha Baraza la Madiwani Cha Chama Cha Mapinduzi kuchagua diwani atakayegombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze kilichofanyika Chalinze ,mapema leo.#KaziInaendelea&nb...

MA DC WAJENGEWA UWEZO KUSIMAMIA UTOAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10

 Na. James Mwanamyoto, OR-TAMISEMI  Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - TAMISEMI Bw. Sospeter Mtwale amesema Wakuu wa Wilaya wanapatiwa mafunzo na Ofisi ya Rais -TAMISEMI ya kuwajengea uwezo wa kusimamia zoezi la utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10 inayotolewa na halmashauri za Wilaya kwa akina mama, vijana na wenye ulemavu.  Bw. Mtwale amesema hayo leo katika Ukumbi wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Kibaha mkoani Pwani kwa Niaba ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - TAMISEMI Bw. Adolf Ndunguru wakati akifungua kikao kazi cha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa na Wakuu wa Wilaya...
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa